Psalms 124

Shukrani Kwa Ukombozi Wa Israeli

(Wimbo Wa Kwenda Juu. Wa Daudi)


1 aKama Bwana asingalikuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:

2 kama Bwana asingalikuwa upande wetu,
wakati watu walipotushambulia,

3 bwakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangalitumeza tungali hai,

4 cmafuriko yangalitugharikisha,
maji mengi yangalitufunika,

5 maji yaendayo kasi
yangalituchukua.


6 Bwana asifiwe,
yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.

7 dTumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tukaokoka.

8 eMsaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
Copyright information for SwhKC